Watanzania maarufu na wasio maarufu waliungana jijini Dar es Salaam Jumanne kusisitiza faida muhimu za mazingira na umuhimu wa juhudi za pamoja za uhifadhi. Tukio hilo lilisisitiza kwamba bila kujali sisi ni nani au tunatoka wapi, sote tunahusiana na mazingira na ni wajibu wetu kuyatunza.
Mwimbaji na mtangazaji wa Televisheni Nakaaya Sumari, waimbaji wawili maarufu Navy Kenzo, na Kiongozi mpya wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika, kutokea Tanzania, Profesa Mohamed Janabi, wote wanatoa sauti zao kuunga mkono mazingira. Kuungwa mkono na watanzania wenye asili mbalimbali, kunatukumbusha juu ya uhusiano wa kina wa kitaifa na kibinafsi ambao sote tunao juu ya mazingira na huduma zake nyingi nzuri - kuanzia uzuri na hamasa, hadi kwenye ajira na afya.
Akizungumza na hadhira iliyokusanyika katika studio za TBC, Sumari alibainisha kuwa mazingira ni Tanzania, na mazingira hayo ni kwa kila mtu. Alihimiza kila mtu kutumia siku nzima kwenye mazingira ya asili na familia zao au marafiki, wakiyathamini na kutafakari juu ya maana yake kwao. Namna nyingine za kuwa mhifadhi zilizopendekezwa na Nakaaya ni kutokula nyama ya mwitu isiyodhibitiwa, kutotupa taka za plastiki mahali ambapo haparuhusiwi, au kufikiria mara mbili kabla ya kukata mimea au miti.
Hassan Sengo, dereva wa boda boda anayeonekana katika video mbili fupi mpya ambazo zitachezwa sana kwenye kituo cha TBC na kwenye mitandao ya kijamii, alisimama kusema kwamba anafaidika na mazingira ya kila siku, kwani kijiwe chake cha boda boda kipo chini ya mti wa mwarobaini ambao hutoa kivuli. Hassan alisisitiza kuwa haijalishi taaluma ya mtu, iwe anaishi kijijini au mjini, mazinigira hutupatia kitu sisi sote.
Pia katika video hizo mpya kuna wasanii wawili maarufu Navy Kenzo. "Tunapata ubunifu wa nyimbo zetu kutoka kwenye mazingira," waimbaji walisema. “Ni muhimu, na kama Watanzania, utambulisho wetu wa kitamaduni, maendeleo ya kitaifa, na matarajio ya baadaye yategemee sana kutumia mazingira kwa uendelevu, na kwa maana hiyo ni lazima sote tuwe wahifadhi. Sisi ni wahifadhi!”
Tanzania na mazingira vimeunganishwa kwa namna ya ndani na ya msingi ambayo haiwezi kutenganishwa. Asili na utamaduni wetu mwingi unatokana na mazingira ya asili, na tuna historia ndefu ya kuishi pamoja kwa uendelevu na mazingira. Mazingira hutoa rasilimali katika mtindo wa maisha yetu na mandhari yetu ya ajabu, na hutoa udongo wetu wenye rutuba na bahari safi. Tanzania ni nyumbani kwa idadi kubwa ya simba ulimwenguni na ya pili kwa idadi kubwa ya tembo, na tunapata karibu 18% ya pato letu la Taifa na ajira milioni 1.5 kila mwaka kutokana na utalii, ambao unaendeshwa sana na utalii. Katika maeneo ya vijijini, mapato yanayotokana na utalii hutiririka moja kwa moja kwenda kwenye jamii kugharamia shule, vituo vya afya na miundombinu.
Ujumbe mkubwa ni: ikiwa wewe ni Mtanzania, una uhusiano na mazingira, unaweza kuchukua jukumu lako mwenyewe katika kuyalinda. Kampeni ya Mimi ni Muhifadhi inalenga kukuza hisia ya uwajibikaji wa pamoja, na kuwahamasisha Watanzania wote kujitambulisha kama wahifadhi. Ni ukumbusho kwamba kuhifadhi mazingira yetu kunanufaisha maisha yetu ya kila siku na ustawi, pamoja na yale ya vizazi vijavyo.
Katika mgahawa wa kahawa jijini Dar es Salaam, mhudumu Neema Mduma aliulizwa mazingira yana maana gani kwake. "Furaha," alijibu.

Kampeni hii inaungwa mkono na Community Wildlife Management Areas Consortium (CWMAC), Honeyguide Foundation na WildAid na inadhaminiwa na Shirika la Utangazaji la Tanzania na Safari Channel.